CHRISS BROWN AOMBA RADHI KWA PICHA ALIYOWEKA AKIVUTA MISOKOTO MITATU YA BANGI

Chris Brown amewaomba radhi fans wake kwa picha yake aliyopost kwenye instagram hivi karibuni ikimuonesha akijipeleka higher na marijuana.

‘Don’t wake me up hit maker’ alikuwa criticised sana na watu baada ya ku-upload picha akivuta misokoto mitatu ya marijuana a.k.a weed kwa wakati mmoja alipotembelea kijiwe kimoja cha wavuta bangi na baadae kupiga picha ambazo aliziweka akiwa na marafiki zake wa kijiweni hapo.
reezy ambae alipost picha akiwa katika ziara yake huko Nertherlands, alifunguka kupitia twitter baada ya watu kuponda sana picha hiyo, tweet yake inasomeka “Oh Amsterdam, wote mnani-treat vizuri sana, namuomba radhi kila mmoja ambae alijisikia vibaya kwa picha yangu ya bangi.” Aliandika Breezy .

Akaona kama haitoshi ikabidi atoe na ushauri pia, “naomba radhi kila mtu lakini kama wote hampendi basi msifanye hivyo pia. Ni rahisi.”

Breezy ambae hivi karibuni ameirudia account yake ya twitter baada ya kuitelekeza kwa muda mrefu kwa sababu ya mgogoro wake na mchekeshaji Jenny Johson, hivi karibuni alitweet message ya kwanza akimaanisha he is back again kwenye mtandao huo wa kijamii na anaanza upya, “ Time to start fresh. #newchapter.” Ilitweet Chris Brown.

Mkali huyo wa R&B aliwashauri pia watu wake ‘team Chris Brown’ kutumia vizuri account ya tweeter kwa kusapoti na kuuza muziki wake na sio kuzungumzia mambo ya relationship abuse.

Una chochote cha kusema juu ya habari hii? Weka comment yako hapo chini.

 

No comments:

Post a Comment